HAKUNA AWEZAYE KUZUIA
MPANGO WA MUNGU JUU YA MAISHA YAKO
Tuanze
kwa kusoma Ayubu(Job 42:2) “Najua ya kuwa waweza kufanya
mambo yote, Na ya kuwa makusudi
yako hayawezi kuzuilika. Haya yalikuwa ni maneno ya Ayubu mcha Mungu baada ya
kupitia majaribu mengi ambayo yalisababisha majeraha na maumivu makubwa katika
maisha yake. Pamoja na misukosuko aliyoipitia Ayubu alisimama imara katika
imani yake na kuzidi kumtumaini Mungu katika yote aliyoyapitia. Wapo ndugu na
jamaa zake wa karibu sana akiwepo mke wake mpendwa ambao kutokana na mateso
ambayo Ayubu aliyapata waliona ushauri pekee ambao ulimfaa Ayubu ilikuwa ni kuacha
kumtumainia/kumcha Mungu. Katika kitabu cha Ayubu 2:9
bibilia inasema “Ndipo
mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu,
ukafe”.
Hii ni kauli inayoashiria kukata tamaa (yaani kukosa tumaini). Hata hivyo kwa
kuwa Imani ya Ayubu kwa Mungu ilikuwa kubwa mno, Ayubu kamwe hakuacha
kumtumainia Mungu na hatimaye alipata ushindi.
Mwisho kabsa tunaona jinsi ayubu alivyobarikiwa kwa Baraka zilizokuwa ni
kuu mno. Katika Ayubu 42:12
bibilia inaandika kuwa “Basi hivyo Bwana akaubarikia huo
mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo kumi na nne elfu,
na ngamia elfu sita, na jozi za ng'ombe elfu, na punda wake elfu.”
Yawezekana nawewe mtu wa
Mungu unapitia katika magumu ambayo kwa namna moja ama nyingne yameleta
majeraha makubwa katika maisha yako. Ndugu ,jamaa na na rafki zako wa karibu
uliowategemea wamekudharau na wamekuona huna msaada wowote katika maisha yao.
Wapo wanaokusengenya na wanaokusimanga kila kuitwapo leo na yawezekana umekata
tama hata ya kuishi. Amini nakuambia kwa kuwa Mungu amekupa fursa ya kuwa hai
mpaka leo na saa hii, tambua kuwa Mungu ana makusudi mema nawewe. Hayo
unayoyapitia unayoyaona kwako yamekuwa ni mzigo usioweza kuubeba kesho
yatageuzwa na kuwa mtaji wako wa kufanikiwa milele.
Ni wangapi ambao
waliomcheka, kumdhihiki na kumtukana Ayubu kwa aliyopitia lakini baadaye
walimwangukia?. Haijalishi ni wangapi waliokuzunguka wakikudhihaki na kukucheka
kutokana nay ale unayoyapitia, ipo siko watakuangukia. Wanaodhani kuwa kwa kuwa wao wamefanikiwa
kwasababu tu wamesoma sana na wewe walikuacha vidato vya nyuma ipo siku
watakuja kuomba kazi kwako. Kwani ni
wangapi ambao hata kidato cha tano na sita hawajafika lakini leo wana
masters. Binafsi nimejifunza kitu cha
msingi kutokana na maisha ya Harith Kapiga ambaye ni mtangazaji wa Clouds fm,
MC na mchungaji ambaye anasema hajawahi soma kidato cha tano wala sita lakini
kwa sasa ana Masters. Ninaamini hata
wewe unaweza kufika mahali pale Mungu alipokusudia iwapo tu utaamua kusimama
imara mahali ulipo pasipo kusikiliza mawazo na maneno ya wanao kukatisha tamaa.
Wema
na fadhili za Mungu ziambatane nawewe siku zote za maisha yako.
Mwandishi:
Patson Mbewa.
1 comment:
SEGA Genesis (Mega Drive) Games: 569 Words - Choegomachine
Play all our SEGA Genesis (Mega Drive) games online in 2019 SEGA Master System / Genesis Model 카지노 A / 파라오카지노 Mega Flashback. Genesis / Model A.
Post a Comment